Image
Image

Mahakama ya Afrika yatoa hukumu ya kesi ya mauaji ya mwandishi Habari za uchunguzi wa Burkina Faso, NORBERT ZONGO.


Mahakama ya Afrika ya  Haki za Binadamu na Watu  yenye makao yake Jijini Arusha  imetoa hukumu juu ya kesi ya mauaji ya mwandishi wa Habari  za uchunguzi  wa Burkina Faso, NORBERT ZONGO  miaka 16 iliyopita.
Katika hukumu hiyo iliyotolewa  mahakama hiyo ime amuru Burkina Faso kuifungua na kuisikiliza upya kesi hiyo iliyohusisha pia mauaji ya watu wengine watatu.
Hukumu hiyo iliyosomwa karibu kwa muda wa saa moja mbele ya jopo la majaji 10 lilokuwa likiongozwa na Jaji Kiongozi,GERARD NIYUNGEKO,ilimuru pia serikali ya Burkina Faso kuchukua jukumu la kuwasaka na kuwapata watuhumiwa wa mauaji hayo.
Mahakama pia imeamuru serikali ya nchi hiyo kuzilipa fidia ya zai di ya dola za Marekani milioni moja , familia za watu hao waliouawa.
Mahakama hiyo iliielekeza serikali ya Burkina Faso kuhakikisha kufanya kila linalowezekana kuwafikisha watuhumiwa husika kwenye vyombo vya sheria ili nao wapa te haki wanayostahili kwa mujibu wa  sheria.
Serikali ya Burkina Faso ilifunga jalada la kesi hiyo mwaka 2006 kwa maelezo ya kukosa ushahidi.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment