Image
Image

News Alert:Mwanamke afanyiwa ukatili wa kutisha kwa kumwagiwa mafuta usoni Songea.


Wakati chama cha waandishi wa habari wanawake(TAMWA) kikilaani  ukatili katika jamii  mwanamke mmoja mkazi wa Sokoine Road mjini Songea mkoani Ruvuma Bi. Rehema Gwaya amefanyiwa ukatili na mke mwenzake kwa kumwagiwa mafuta ya moto usoni na kuungua   sehemu mbalimbali  za mwili wake.
Bi. Rehema Gwaya ambaye amelazwa katika Hospitali ya mkoa Songea akiwa na mwanae wa miezi saba anasema chanzo cha kufanyiwa ukatili huo ni kutofautiana na mke mwenzake aitwaye Zefania Chimgege baada ya kuhoji masuala ya usafi  ambapo Zefania aliyekuwa akipika maandazi akamwagia karai la mafuta ya moto usoni.
Baada ya kufanyiwa unyama huo shemeji yake ambaye ni mume wa Zefania Bw.Hafidhi Hamidu Mbaya akamwambia atoke nje ammalizie kwa kumchoma na kisu.
Mganga mfawidhi katika hospitali ya mkoa Songea(HOMSO) Dkt.Benedikt Ngaiza anaelezea hali ya mgonjwa huyo huku wakazi wa songea wakilaani ukatili huo.
Rehema Gwaya na Zefania Chimgege wameolewa sehemu moja na wote wanaishi katika nyumba ya baba Mkwe na waume zao na kwamba zefania chimgegeanashikiliwa na polisi kwa kufanya ukatili huo.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment