Image
Image

Wamarekani hawampendi tena Hillary Clinton.


Televisheni ya Marekani ya CNN, imetangaza kuwa idadi kubwa ya raia wa nchi hiyo, hawampendi tena Hillary Rodham Clinton, Waziri wa zamani wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo na ambaye pia ni mgombea urais katika uchaguzi wa mwaka kesho, kwa tiketi ya chama cha Democrati nchini humo.
Kwa mujibu wa kanali hiyo, raia wa Marekani hawana imani na Clinton na kwamba suala hilo liko wazi sana. Uchunguzi uliofanywa na televisheni hiyo unaonyesha kwamba,  asilimia 57 ya wananchi wa Marekani wana mtazamo hasi na shakhsia huyo, huku asilimia 52 ya nyingine ikimtaja kuwa asiyeyapa umuhimu matatizo ya raia wa kawaida.
Aidha uchunguzi huo umeongeza kuwa, raia wengi wa Marekani hawakuridhia utendaji kazi wa waziri huyo wa zamani wa mambo ya nje wa Marekani mwaka 2012 suala ambalo limepunguza uungaji mkono wa wananchi kwake.
Hii ni katika hali ambayo uchunguzi wa hapo kabla wa kanali hiyo ya televisheni, ulikuwa umemtangaza bibi huyo kuwa mwenye mvuto kwa ajili ya mchuano wa uchaguzi wa mwaka 2016 nchini Marekani.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment