Image
Image

News Alert:Wafugaji waandamana hadi kwa mkuu wa wilaya Tunduru.


Baada ya  amri ya wafugaji  kutakiwa kuondoka ndani ya siku tatu  iliyotolewa na  uongozi wa Halmashauri ya Wilaya Tunduru Mkoani Ruvuma   wafugaji hao wameandamana hadi kwa  Mkuu wa Wilaya ya Tunduru wakiomba kutafutiwa maeneo mengine  wilayani humo.
Wafugaji hao  wenye ngo'mbe  Elfu-38  walifika Wilayani Tunduru  mwaka 2006 wakitokea Ihefu  Mkoani Mbeya wanasema wao hawakataki kuhama bali wanataka Serikali  iwaon eshe kwa  kwenda .
Wafugaji hao wameamua  kuandamana  hadi kwenye ofisi ya mkuu wa Wilaya ya Tunduru kufuatia kauli  ya Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya  ya Tunduru ,Bwana   FARIDU HAMIS kuwataka kuondoka  ndani ya siku tatu .
Katibu wa  Chama  cha  Wafugaji  Kanda  ya Kusini ,Bwana CORNERY  KAPINGA ameiomba Serikali kuwatengea maeneo  miongoni mwa mapori mengi katika Wilaya ya Tunduru .
Kwa upande wake  Mkuu wa Wilaya ya Tunduru anayehamia Wilaya ya Namtumbo , Bwana CHANDE BAKARY NALICHO ameoongeza muda  wa wafugaji hao  kuondoka kwenye maeneo tengefu na kando ya Mto Ruvuma     na  wakitakiwa kufuata taratibu katika maeneo watayokubaliwa na wanakijiji.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment