Image
Image

Wananchi wanatembea umbali wa zaidi km 10 kutafuta huduma za afya.


Wananchi wa kijiji cha kiti cha mungu wilaya ya Mwanga mkoani kilimanjaro wamelalamikia tatizo la ukosefu wa vipimo na dawa katika zahanati ya kijiji  hicho licha ya kuchangishwa fedha kiasi cha shilingi elfu kumi kwa ajili ya huduma za bima ya afya.
Wananchi wa kijiji hicho wanasema wanawake na watoto ndiyo wanateseka zaidi na kwamba wakifika katika zahanati hiyo hawapati huduma za afya badala yake wanapewa karatasi kwenda kununua dawa.
Kwa hali hii wanadai imekuwa kero hali ambayo inawakatisha tamaa ya kuendelea kuchagia fedha kwa ajili ya bima ya afya na kwamba wameshatoa malalamiko ngazi ya wilaya bila mafanikio sababu ambayo kwa sasa inayowalazimu kutembea umbali wa zaidi km 10 kutafuta huduma za afya.
Mganga wa zahanati ya kijiji cha kiti cha Mungu Dkt.Chard  Mshana amekiri kuwepo kwa tatizo hilo na kusema kuwa dawa zinazoletwa katika kijiji hicho ni kidogo sana ikilinganishwa na idadi ya wananchi wanaohitaji huduma za afya.
Akijibu malalamiko hayo mkurugenzi wa halmashuri ya wilaya ya mwanga Bw.Jamuhuri Wilium ameahidi kufuatialia tatizo hilo na kulitafutia ufumbuzi kwenye  kamati za afya za wilaya ambazo zinahusika kusambaza dawa katika zahanati .
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment