Image
Image

News Alert:Wahamiaji haramu wakamatwa wakijiandikisha kwenye daftari la wapiga kura Kigoma.


Watu ishirini wanaosadikiwa kuwa wahamiaji kutoka nchi jirani wamekamatwa mkoani kigoma baada ya kujiandikisha katika Daftari la kudumu la wapiga kura, katika uandikishaji wapiga kura kwa kutumia mfumo wa kielektronik BVR unaoendelea mkoani kigoma.
Mkuu wa mkoa wa kigoma Luten Kanal mstaafu Issa Machibya amesema wakati wa ibada ya kanisa la kiinjili la kilutheri tanzania mission ya kigoma iliyoambatana na harambee ya ujenzi wa shule ya msingi ya kanisa hilo mjini kigoma, kuwa watu hao ambao wamejaribu kujiandikisha tayari wamefikishwa mahakamani.
Kutokana na hali hiyo ametoa onyo na kuahidi kuwachukulia hatua kali zaidi  ikiwa ni pomoja na watanzania watakaobainika kuwasaidia wahamiaji kujiandikisha.
Kwa upande wake   askofu mkuu wa kanisa la kiinjili la kilutheri tanzania KKKT nchini DR  ELEX  MALASUSA amesema moja ya kazi za kanisa hilo ni kuhakikisha jamii inaelimika na kufuata mafundisho ya mwenyezi mungu ambapo akizungumzia ujio wa wakimbizi kutoka burundi ametaka wasaidiwe ikiwa ni pamoja na kuiombea nchi hiyo ili ipate amani.


Katika  harambee  hiyo ya ujenzi wa shule ya msingi, zaidi ya shilingi milioni 53 ikiwa ni pesa taslimu na ahadi  zimepatikana.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment