Image
Image

Prof.Gerald:Katika kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi tafiti zinatakiwa kutumika katika jamii kuinua uchumi.


MAKAMU Mkuu wa Chuo cha Sokoine cha Kilimo (SUA) Prof.Gerald Monella amesema katika kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi katika kilimo,tafiti za kisayansi zinazofanywa na watafiti zinapaswa kutumika katika jamii ili kuweza kuinua uchumi wa nchi.
Akifungua mkutano wa Kimataifa wa Mabadiliko ya Hali ya Hewa na Kilimo endelevu katika nchi za Afrika,(Climate change and Multi-Dimensional sunstanability in Africa Agriculture),Pro.Molella amesema tafiti hasa za kilimo zinapaswa kupewa nafasi katika sekta ya kilimo hapa nchini.
Amesema mkutano huo,ambao SUA ndio wenyeji unashirikisha wadau mbalimbali wa kilimo kutoka nchi za Afrika na watajadiliana fursa ya kilimo endelevu katika uchumi,jamii na mifumo ya taasisi
Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi wa Mradi wa Tafiti Bunifu za Kilimo,(IAGRI)Pro.Isaac Minde amesema katika mradi wao wanafundisha vijana juu ya namna ya kufanya utafiti katika hali ya ubora zaidi ili kuweza kupambana na changamoto za kilimo katika maeneo yao,nia ikiwa kuhakikisha kilimo endelevu kinapata nafasi ya kuinua uchumi wa nchi na namna ya kupambana na mabadiliko ya hali ya hewa kila msimu wa kilimo.
Naye mdau wa Kilimo,Mkuu wa Mkoa wa Singida,Paresko Cone,amesema tafiti zinazofanywa katika kilimo hazina budi kutumika kuisaidia jamii kuweza kuwa na uwezo wa kuzalisha kila msimu na kuweza kutokomeza njaa ndani ya jamii.
Amesema kinachotakiwa katika sekta ya kilimo ni viongozi wanaongoza na jamii kuwa wabunifu,kuthubutu,kwani hakun lisilowezekana katika kupambana na mabadiliko ya hali ya hewa kwani mkoa wa singida wametumia tafiti za kilimo zilizofanywa SUA na kuzitumia na mpaka sasa mkoa huo una chakula cha kutosha kwa kila msimu.
Pia amesema mkoa wa singida kwa sasa hakuna tena migogoro ya ardhi kutokana na mkoa huo kuwa na mpango bora wa matumizi ya ardhi,mkulima na mfugaji wametengewa maeneo yao na hakuna anayemwingilia mwingine katika eneo alilopangiwa.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment