Image
Image

Rais OMAR HASSAN Al-BASHIR wa Sudan hawezi kukamatwa wakati akiwa Sandton.


Rais OMAR  HASSAN  Al-BASHIR wa Sudan hawezi kukamatwa wakati akiwa Sandton,Afrika  Kusini unapofanyika  mkutano wa viongozi wa Umoja wa Afrika kwani eneo hilo kwa sasa liko chini ya mamlaka ya Umoja wa  Afrika.
Taasisi ya Masuala ya Kimataifa ya Afrika Kusini imesema kama inavyofahamika Umoja wa Afrika unafanya mkutano wake hapo eneo ambalo limetangazwa kama  eneo la Umoja huo kwa mujibu wa  kanuni za kimataifa.
Kwa sababu hiyo msemaji wa taasisi hiyo,Bwana HOPEWELL RA DEBE amesema polisi wa Afrika  Kusini  hawawezi kwenda mahali hapo na kumkamata mtu yeyote wakati wa kipindi cha mkutano huo ulioanza jana na unatarajia kukamilika  leo.
Amesema Serikali ya Afrika   Kusini ilijua hali hiyo kwamba suala  la Rais BASHIR lingeibuliwa na  mashirika ya kimataifa na makundi mengine ya ushawishi na ndiyo ime jitokeza Mahakama ya Uhalifu ya  Kimataifa ya ICC ambayo imekuwa inamtafuta kwa muda mrefu ku taka Afrika ya Kusini ambayo ni  mwanachama wa mahakama hiyo imkamate kitu ambacho hakiwezekani.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment