Image
Image

Vyama vya siasa vyatakiwa kutetea usawa katika uteuzi wa wagombea nafasi za uongozi.


Mtandao wa Wanawake na Katiba Tanzania utashawishi wanawake nchini na wale wa makundi ya pembezoni kutounga mkono chama chochote cha kisiasa kisichotetea ajenda ya kuinua maisha na kulinda utu wa wanawake, ambacho hakitaonyesha ari ya dhati ya kuteua wanawake kuwania nafasi mbalimbali wakati wa uchaguzi na kile ambacho viongozi wake wanadharau haki ya msingi ya kujenga usawa wa jinsia.
Mtandao huu unaounganisha asasi za kiraia takriban 65 na watu binafsi watetezi wa haki za wanawake, watoto na makundi yaliyoko pembezoni, umekuwa ukifuatilia mwenendo wa vyama vya siasa hasa kwa wanaotangaza nia ya kugombea uongozi katika ngazi ya uraisi, ubunge, baraza la uwakilishi na udiwani na kubaini kuwa baadhi ya vyama vimeshindwa kuteua wanawake kuwania nafasi mbalimbali ndani ya nchi.
Katika ufuatiliaji huo, Mtandao wa Wanawake na Katiba umepata wasi wasi wa kutokuwepo kwa watangaza nia wanawake wala kusikika kwa ajenda ya kuimarisha ukombozi wa kimapinduzi wa wanawake wakati huu wa hatua za awali za uteuzi wa viongozi wa kisiasa ndani ya vyama.
Aidha Mtandao umebainisha kutokuwepo uzingatiaji wa misingi inayopelekea kuwepo kwa usawa wa jinsia katika mchakato wa kuteua wagombea ndani ya vyama vya siasa ambavyo vimeshateua wagombea ambapo hakuna hata mwanamke mmoja aliyeteuliwa. 
Mtandao umeliona jambo la kutoteuliwa kwa wanawake katika ngazi za awali ndani ya vyama ni kinyume cha msingi wa kujenga, kukuza  na kuimarisha demokrasia ya chama na nchini kwa ujumla.
Mtandao umewataka viongozi na wanachama wa vyama yva siasa, na wale wanaotangaza nia kubeba ajenda ya kuongeza ushiriki wa wanawake katika ngazi za maamuzi katika kupambana na masuala yanayowagusa moja kwa moja yakiwemo kutokulindwa kwa utu wao, kuondoa ukatili wa kijinsia, kupinga mila potofu kama vile ukeketaji na ndoa za utotoni, umiliki wa raslimali za nchi, pamoja na suala zima la kuhakikisha kuwa wanawake wanapata haki sawa katika nyanja za kisiasa, kiuchumi na kijamii.
Valerie N. Msoka
Mkurugenzi Mtendaji

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment