Image
Image

Wanafunzi 270 wa Chuo cha Ualimu Korogwe wanakabiliwa na ukosefu wa maji chuoni hapo.


Wanafunzi 270 wa Chuo cha Ualimu Korogwe ,waliochaguliwa na Serikali kusomea Stashahada ya Juu ya Sayansi na Hisabati kwa lengo la kupunguza uhaba wa walimu wa masomo hayo nchini,wanakabiliwa na  matatizo mbali mbali ikiwemo ukosefu wa maji chuoni hapo hatua waliyoielezea kuwa inaweza kusababisha magonjwa ya milipuko.
Wakizungumza  chuoni hapo  wakati viongozi wa Serikali wa  wilaya na mkoa wa Tanga  walipotembelea na  kukabidhiwa vifaa vya ujenzi vilivyotolewa na Hifadhi  z a Taifa  - TANAPA - kupitia Hifadhi ya Mkomazi kwa lengo la kuwapunguzia  matatizo  wanafunzi hao,wamesema mbali na ukosefu wa maji pia wameathirika kiuchumi hivyo wameikumbusha Serikali kutekeleza ahadi yake ya kuwapatia mikopo   ili wajinunulie  vifaa v itakayowawezesha kusoma kwa ufanisi .
Kuhusu mikopo msemaji wa wanafunzi hao,LOTAMWANG'AKI MOLLEL amesema kuna ahadi iliyotolewa na Katibu Mkuu Wizara  y a Elimu na Mafunzo ya Ufundi ,Profesa SIFUNI MCHOME kuwa wa tawezeshwa mikopo ili wafikie malengo yao kwa ufanisi.
Kufuatia hatua hiyo Mkuu wa chuo hicho ,Bwana  JAM ES MMBAJI amesema chuo kina kisima cha maji ambayo yanatoka muda wote ,lakini hayatoshelezi mahitaji.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment