Image
Image

Wananchi wa mkoa wa Kilimanjaro wanakunywa maji ya bwawa Kutokana na uhaba wa Upatikanaji wa huduma ya maji safi.


Wananchi wa  vijiji  18 vya  Kata ya Kiria Wilayani Mwanga Mkoani Kilimanjaro  wanakabiliwa na tatizo la upatikanaji wa huduma ya maji safi hali inayowalazimu kunywa maji ya bwawa la Nyumba ya Mungu ambayo ni hatari kwa usalama wa afya zao.

Wananchi hao wamesema wanalazimika kunywa maji hayo kutokana na kukosekana kwa maji maeneo ya  karibu na makazi ya wananchi hao wa ukanda wa tambarare .

Wamesema tatizo hilo linasababisha wakazi wa vijiji vya Kata hiyo kuugua magonjwa ya mlipuko kila mwaka  na kwamba wamekuwa wakipewa ahadi za kuletewa  maji kwa muda mrefu bila mafanikio .

Mwenyekiti wa Kijiji cha Kiti cha Mungu , Bwana   EDIMUNDU MWAIPUNGU  ame sema maji hayo ya bwawa hilo ni hatari kwa afya za binadamu kutokana na bwawa hilo  kupokea maji machafu kutoka maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Kilimanjaro

Mkurugeznzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mwanga , Bwana  JAMUHURI WILI AM anakiri kuwapo kwa tatizo hilo na kwamba kuna mradi unaotekelezwa  kupeleka maji katik a kata hiyo ambao tayari umesha anza  na kwamba endapo utakamilika utaondoa adha kwa wananchi wa vijiji 18 vya wilaya hiyo .


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment