Image
Image

Watu 68 wamekufa kusini mwa Nigeria kwa kunywa pombe kali ya kienyeji yenye sumu.


Watu 68 wamekufa kusini mwa Nigeria kwa kunywa pombe kali ya kienyeji yenye sumu iliyopigwa marufuku na maafisa wa afya.
Afisa wa Wizara ya Afya katika Jimbo la Rivers State DR. SIMEON IBUFUBARA MANEUL amesema watu hao wamekufa tangu tarehe 31 ya mwezi uliopita na kwamba watu 38 wamekufa baada ya Jumanne wiki hii wakati maafisa walipopiga marufuku utengenezaji na unywaji wa pombe hiyo ya kienyeji inayoitwa Ogogoro.
Pombe hiyo hutengenezwa kwa utomvu wa miti ya mitende kama tembo lakini kwa kawaida huchakachuliwa kwa kuwekwa  ethanol inayoongeza ukali wa  p ombe kufikia viwango vya asilimia 60.
Maafisa wa afya wanasema mamia ya watu hufa kila mwaka kwa aina ya pombe hiyo na kwamba mlipuko wa vifo vya hivi karibuni ulianza wakati wa sherehe kwenye mgahawa mmoja unafahamika sana kwa supu ya mbwa.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment