Image
Image

CHADEMA yawataka wananchi kuwaunga mkono ili kuweza kuwakomboa.


Chama cha Demokrasia na Maendeleo -CHADEMA- kimewataka wananchi kukiunga mkono chama hicho katika harakati zake za kuwakomboa watanzania  kuepukana na kupata wimbi la viongozi  wenye  ubinafsi  wasio  na  uadilifu  wakati  huu wa kuelekea  uchaguzi  mkuu  ambapo  idadi  kubwa  ya wanaosaka madaraka  wamekuwa  wakipita  huku  na  huko  kuwarubuni  wananchi.
Akizungumza na wakazi  wa  Wilaya ya Urambo katika mkutano wa hadhara, Mkurugenzi wa Ulinzi na usalama wa  CHADEMA , WILFRED LWAKATARE  amesema  wataendelea   kuwaeleza ukweli  wananchi  hatua ambayo itasaidia kuwafumbua macho  kuhusu wimbi la wanaosaka madaraka  hasa   kupitia  Chama cha  Mapinduzi  kuwa  hawana ukweli  wa  kuwasaidia  wananchi.
Katika hatua nyingine  wakati  akifunga  mafunzo ya vijana  Red Brigedi  wa  CHADEMA  wapatao  mianane wilayani  Urambo  Mkurugenzi  huyo  wa Ulinzi  na Usalama  amewataka  vijana  hao  kuwa makini  na baadhi  ya  wanasiasa  wanaotaka kuwatumia  wakati  huu wa kuelekea  uchaguzi  mkuu.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment