Image
Image

OBAMA aionya iran,Asema nchi yake itajiondoa kwenye mazungumzo ya nyuklia na nchi hiyo ikikiuka makubaliano.


Rais BARACK OBAMA  ameonya kuwa nchi yake  itajiondoa kwenye mazungumzo  ya mpango wa nyuklia wa Iran iwapo  Iran itakiuka mpango uliokubaliwa Aprili  mwaka huu Lausanne, Uswis, lakini amesema ana matumaini kuwa mazungumzo yanayoendelea yatafanikiwa.
Amesema bado kuna masuala muhimu ya kujadiliwa lakini suala  hilolipo kwa upande wa Iran kukubaliana na matakwa yaliyowekwa na mataifa matano makubwa Aprili mwaka huu.
Rais OBAMA ameyasema hayo kwenye  mkutano wa waandishi wa habari Mjini Washington akiwa na Rais wa Brazil Bi DILMA ROUSSEFF anayeizuru Marekani.
Kauli ya Rais OBAMA imekuja baada ya Rais wa Iran Bwana HASSAN ROUHANI pia kuonya  nchi yake  itarejea katika shughuli zake za mpango wa nyuklia iwapo mataifa matano makubwa duniani yatakiuka makubaliano.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment