Afisa mmoja wa Polisi,AGUSTINUS
TARIGAN amewaambia Waandishi wa Habari leo asubuhi kuwa miili ya watu 141
imepatikana kutoka eneo ilikoanguka ndege hiyo.
Jeshi la nchi hiyo limesema hakuna
mtu aliyenusurika miongoni mwa watu 122 waliokuwemo kwenye ndege hiyo Hercules C-130, ilipogonga nyumba
na hoteli na kisha kuwaka moto.
Taarifa imesema wengi wa watu
waliokfua inaaminika kuwa ndugu wa
wanajeshi na taarifa za hivi karibuni zinasema watu 19 wamekufa ardhini ambako
ndege hiyo imenguka.
Chanzo cha kuanguka kwa ndege hiyo
hakijajulikana, lakini walioshuhudia tukio hilo wanasema inaeleke ilikumbwa na
tatizo muda mfupi baada kuruka kutoka uwanja wa ndege wa Mji wa Medan, ambao ni
mji wa tatu kwa ukubwa nchini Indonesia.




0 comments:
Post a Comment