Image
Image

Madaktari bingwa kutoka Ubelgiji kuwatibu Mtoto wa Jicho wakazi wa Kilimanjaro.


Wakazi wa Mkoa wa Kilimanjaro wenye matatizo ya macho wamejitokeza kwa wingi katika hospitali ya rufaa ya mkoa huo MAWENZI - kupata huduma ya matibabu na upasuaji wa mtoto wa jicho inayotolewa na madaktari bingwa kutoka Ubelgiji bila ya malipo.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa huduma hiyo inayofadhiliwa na Lions Club,  MRAtibu wa Lions Club ya Kibo Kilimanjaro,  Bwana NITU REHAL amesema madaktari hao bingwa watatoa  huduma bure kwa watu wote wenye matatizo ya macho katika Wilaya za Moshi, Hai na Siha na watoto wenye albinism.
Amesema madaktari hao wanatoa huduma hiyo kwa kushirikiana na madkari wa macho Mkoani Kilimanjaro kwa siku kumi na kwamba ni vema wananchi wenye matatizo ya macho hasa ususani maeneo ya vijijini kujitokeza kupatiwa vipimo, matibabu na wale wenye tatizo la kuchunwa na kufanyiwa upasuaji.
Kwa upande wake Raisi wa Madaktari bingwa wa macho kutoka Shirika la See and Smile nchini Ubelgiji,  Dakta  CLAEYS MARNIX amesema kwa siku wanahudumia watu 250 na kwamba mpaka sasa wengi waliofanyiwa vipimo wamebainika kuwa na tatizo la mto wa jicho pamoja na trakoma.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment