Image
Image

Wanafunzi waitaka serikali kutatua tatizo la uhaba wa waalimu wa masomo ya Sayansi Shinyanga.


Wanafunzi wanaosoma mchepuo wa Sayansi katika shule za sekondari mkoani shinyanga wameitaka serikali kufanya juhudi za kutatua tatizo la  uhaba wa waalimu wa masomo hayo.
Wamesema maabara zinazojengwa kwa agizo la Rais JAKAYA KIKWETE halitakidhi haja na vigezo muhimu kutokana na ukosefu wa walimu,  hali itakayoifanya Tanzania kushindwa kufanya mabadiliko ya teknolojia na kusababisha taifa kushindwa kuingia katika soko la ushindani wa ajira duniani.
Hayo yamesemwa na wanafunzi  wa masomo ya sayansi katika shule za sekondari Old Shinyanga, Mazinge, Ngokolo na Kizumbi wakati wa hafla ya kupokea maabara nne zilizojengwa na kampuni ya ACACIA inayomiliki mgodi wa dhahabu wa Buzwagi.
Kwa upande wake meneja wa kampuni ya ACACIA Buzwagi Bwana PHILBERT ROYMAM amesema lengo la kampuni yake ni kuhakikisha maabara hizo zinakuwa chachu ya kupatikana wataalamu wa uhakika watakaoweza kuleta maendeleo.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment