Image
Image

Idadi ya makada wa CCM yaongezeka katika kurudisha fomu za kuomba udhamini wa kugombea nafasi ya urais.


Ikiwa imesalia siku moja kwa makada wa chama cha mapinduzi kurudisha fomu za kuomba udhamini wa kugombea nafasi ya urais  idadi ya wanaorudisha imeongezeka maradufu huku homa ya kinyang'anyiro hicho ikizidi kupanda kuelekea mkutano mkuu utakaofanyika july 12 ambao ndio utamchagua mgombea wa urais kupitia ccm.
Miongoni mwa makada waliorudisha fomu hizo ni pamoja na waziri mkuu mstaafu Mhe Edward Lowassa ambaye ameambatana na maelfu ya wafuasi na kufanya viwanja vya makao makuu ya ccm kufurika watu ambapo amesema ana shauku kubwa ya kuunganisha nguvu na uwezo wa kila mtanzania katika kupambana na umasikini kwani umasikini kamwe sio amri ya mwenyezi mungu.


Kada mwingine ni naibu waziri wa fedha mhe Mwigulu Nchemba ambaye pamoja na mambo mengine amesema endapo atapewa ridhaa na wana cch na kisha watanzania wakamchagua kuwa kiongozi wao atahakikisha anakabiliana na rushwa iliyokithiri na kutatua tatizo sugu la ajira hasa kwa vijana kwa kuongeza fursa za ajira na uwekezaji.

Lazaro Nyalandu waziri wa utalii ambaye na yeye amejitosa katika kinyang'anyiro hicho naye pia amerudisha fomu akiomba ridhaa ya kuteuliwa kuwania urais huku ambaye pamoja na mambo mengine ameahidi kuinua uchumi wa nchi utakaotegemea rasilimali zilizoko nchini kwa manufaa ya wate.
Dk Hass Kitine mkurugenzi wa zamani wa idara ya usalama wa taifa ni miongni mwa makada waliotupa turufu yao kuwania nafasi hiyo ya juu ya uongozi kupitia ccm huku akitilia msisitizo suala la utawala bora unaozingatia miiko na maadili ya uongozi akiwa na imani kuwa mambo hayo ndio msingi wa maendeleo wa taifa lolote lile duniani lililopiga hatua kiuchumi.
makada wengine waliojitokeza hii leo ni pamoja na Dk .Hamis Kigwangala mbunge wa nzega ambaye amesema imefika wakati sasa taifa kupunguza mamlaka za uteuzi hasa katika nafasi ya urais ili kuongeza uwajibikaji huku idadi kamili ya waliorudisha fomu hadi hvi sasa ikiwa ni kati ya makada 41 waliojitokeza. 
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment