UONGOZI wa Simba umesema mchezaji wa zamani wa Yanga, Hamis Kiiza
atajiunga na klabu hiyo kwenye mazoezi kati ya leo au kesho iwapo tu
atafuzu vipimo vya afya.
Kiiza, ambaye alitemwa Yanga msimu uliopita, alitarajiwa kuwasili
wakati wowote kuanzia jana, na leo atapimwa afya ili kuungana na
wachezaji wengine wa Simba katika mazoezi.
Akijibu maswali ya waandishi wa habari jana, Rais wa Simba Evans
Aveva alisema Kiiza atakuwa mchezaji halali wa Simba iwapo atafuzu
vipimo leo.
“Kiiza atatua muda wowote kuanzia leo (jana) na akifaulu vipimo vya afya moja kwa moja atakuwa mchezaji wetu,”alisema.
Mchezaji huyo Mganda alitemwa na aliyekuwa Kocha wa Yanga, Mbrazili
Marcio Maximo msimu uliopita na nafasi yake kuchukuliwa na Kpah Sherman.
Kiiza hivi karibuni alinukuliwa kwenye vyombo vya habari akithibitisha
ujio wake wa kujiunga na Simba.
Iwapo atafanikiwa kusajiliwa Simba atatimiza jumla ya wachezaji wanne
wanaotoka Uganda baada ya Emmanuel Okwi na Simon Sserunkuma na Juuko
Murshid huku Raphael Kiongera akitokea Kenya.
Katika hatua nyingine, Aveva alisema atatangaza rasmi kambi ya maandalizi ya msimu kabla ya kumalizika kwa wiki hii.
Alisema kocha mpya wa mazoezi ya viungo, Dusan Momcilovic na makipa
Abdul Salim wataungana na kikosi cha Simba leo kwenye mazoezi kuanza
kazi rasmi.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)


0 comments:
Post a Comment