MS H A M B U L I A J I mpya wa Yanga, Mzimbabwe Donald Ngoma,
amewataka mashabiki wa timu hiyo kusubiri mambo mazuri kutoka kwake
ikiwa ni muda mfupi baada ya kusaini mkataba wa miaka miwili kuichezea
timu hiyo.
Ngoma aliyetambulishwa rasmi jana kwenye makao makuu ya klabu ya
Yanga sambamba na beki Mghana Joseph Zuttah, alisema amejipanga kufanya
kazi kubwa na kuipa mafanikio timu hiyo ili aweze kudumu kwa muda mrefu
kama ilivyokuwa FC Platinum.
“Najisikia furaha kucheza Yanga kwa sababu ni klabu kubwa Tanzania
nitahakikisha natumia uwezo wangu, naongeza mafanikio yaliyopo kwa
kushirikiana na wenzangu niliowakuta,”alisema Ngoma.
Kwa upande wake, Zuttah alisema ametua Yanga kwa kazi moja tu ya
kuendeleza mazuri yaliyofanywa siku za nyuma na amekuja akiwa kamili na
kuwataka washabiki wa timu hiyo kumpa sapoti.
“Nimefurahi kuona mashabiki wanaipenda sana timu yao kuanzia Jumamosi
wakati Yanga ilipocheza na Sports Club Villa nimehamasika sana kitu
ambacho kimenifanya nisijutie maamuzi yangu ya kucheza Tanzania,”alisema
Zuttah.
Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Yanga, Jerry Muro wachezaji hao
wameshamalizana nao kila kitu na tayari wameshawasilisha usajili wao
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), ili waweze kuombewa kibali cha
kufanyia kazi.
Ngoma ametua Yanga aki tokea FC Platinum ya Zimbabwe wakati Zuttah
alikuwa akikipiga klabu ya Medeama ambao ni mabingwa wa Kombe la FA
nchini Ghana.
Baada ya kuwanasa wachezaji hao wawili, tayari Yanga imekamilisha
idadi ya nyota saba wa kimataifa inayotakiwa kwa mujibu wa kanuni za
TFF, ambapo wengine ni Haruna Niyonzima, Amissi Tambwe, Kpah Sherman,
Andrey Coutinho na Mbuyu Twite.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)


0 comments:
Post a Comment