Image
Image

TFF iache ubaguzi kwa wachezaji wadogo.

Viongozi wa shirikisho la soka nchini TFF wametakiwa kuacha kuwabagua vijana wadogo wenye vipaji wanao patikana katika mashindano mbali mbali yanayoendeshwa kwani kwa kufanya hivyo kumekuwa kukikatisha tamaa kundi hilo na morali ya kufanya zaidi mazoezi.

Hayo yamebainishwa na vijana kutoka taasisi ya kukuza vipaji ya Moro KIDS ya mkoani Morogoro wakati wa mazoezi ya mchezo wa soka ambapo vijana hao wamesema kitendo cha TFF kutowatumia vyema vijana kutoka taasisi mbali mbali za kuibua vipaji ikiwemo kuwashirikisha kucheza katika timu ya taifa kumesababisha Tanzania kuendelea kufanya vibaya kwenye mashindano mengi ya kimataifa huku kocha wa timu hiyo ya vijana hussein mau akibainisha baadhi ya changamoto wanazokutana nazo.

Katika mchezo wa masumbwi kocha mkongwe wa mchezo huo mkoa wa Morogoro, Pawa Iranda ametoa wito kwa raisi atakayechaguliwa,sambamba na wadau wengine wa mchezo huo kuupa sàpoti mchezo wa ngumi ikiwemo kusaidia mahitaji mbali mbali kama udhamini na vifaa ili kuweza kuufikisha mbali mchezo na kuitangaza nchi kimataifa kama alivyoweza  kuipeperusha vyema bendera ya tanzania ndani na nje ya nchi bondia wa ngumi za kulipwa Francis Cheka na mabondia wengine.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment