Image
Image

Unafahamu Asali ni msaada mkubwa katika kuimarisha afya,Soma hapa.

Hizo zikiwa ni faida za fenesi hebu sasa tueleze faida za asali,Asali hutengenezwa na nyuki na bila shaka karibu sote tunaelewa kuwa chakula hicho cha asili ni kina faida nyingi.
Wataalamu wanatuambia kuwa,nyuki ana uwezo wa kutembea maili elfu tatu akikusanya nta za maua ya aina mbalimbali kutoka katika miti mbalimbali inayoweza kufikia milioni kumi na tano kwa ajili ya kutengeza asali kilo moja ndani ya miezi mitatu. 
Kutokana na mchanganyiko huu unaotengenezwa na mdudu nyuki,asali ina uwezo wa kutibu magonjwa zaidi ya mia moja.
Kwa sababu hiyo ni bora tukijizoesha kutumia asali badala ya sukari katika vinjwaji na vyakula mbalimbali hasa kwa kuwa sukari inaweza kuwa na kemikali zenye madhara kwa miili yetu. 
Tunashauriwa kutumia asali kama kiungo katika chai,uji,maziwa na katika vinywaji mbalimbali badala ya sukari. 
Baadhi pia hutumia asali kama kitoweo kwa kulia ugali uliopoa.
Si vibaya ukijua kuwa,ukila asali na ugali wa moto unaweza kupata maumivu ya tumbo.
Tunashauriwa kutumia asali kwa wingi kwani pia ni 'antibiotics'.Kumbuka kuwa,asali mbichi ambayo haijachemshwa motoni ndiyo inayofaa.
Sukari iliyoko kwenye asali humeng'enyuka kwa urahisi sana na kugeuka kuwa glukosi na fruktosi ambayo huingia kwenye damu mwilini haraka sana ikilinganishwa na vimiminika vingine kama maji ya kawaida. 
Asali husaida pia figo na utumbo kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa.
Asali pia ina kalori chache sana na ukilinganisha na kiwango cha sukari ilichonacho,cha ajabu ni kuwa hutoa nishati nyingi katika mwili lakini haisababishi ongezeko la mwili yaani unene kwa urahisi. 
Hata hivyo tunausiwa kuwa tukitumia asali kiholela na kuila kwa wingi nayo pia huweza kusababisha unene kama ilivyo sukari.
Faida nyingine za asali ni kusaidia utengenezaji wa damu mwilini, kusafisha damu na kusaidia mzunguko wa damu kuwa rahisi na mwepesi. 
Halikadhalika asali husaidia mishipa ya damu isiathirike na maradhi yanayoshambulia mishipa hiyo. 
Pia husaidia ubongo na kuuweseha kufanya kazi vizuri na upesi zaidi. 
Faida nyingine ya asali ni kusaidia kuua bakteria wa aina mbalimbali inapotumiwa kwa matibabu na hasa kwenye vidonda. 
Pia asali husaidia kuondoa matatizo ya tishu yaani tissue difficiency na udhaifu kwenye mwili.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment