Image
Image

8 wafariki katika shambulio la bomu Afghanistan.



Lori la bomu lalipuka katikati mwa jiji la Kabul nchini Afghanistan leo ikiwa ni siku ya ijumaa.Repoti iliyotolewa na polisi na maafisa wa idara ya afya imeonyesha kwamba mamia wamepata majeraha na watu 8 kupoteza maisha yao.

Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na mashahidi wa tukio hilo waliripoti kuwa eneo moja ililipuliwa na kusababisha shimo lenye kina kirefu cha mita 10.

Majumba kadhaa yaliharibika kutokana na mlipuko huo.

Waziri wa afya wa Afghanistan alifahamisha kuwa taarifa hiyo ilitolewa na hospitali ambazo ziliwapokea majeruhi kwa ajili ya matibabu.

Waziri huyo alifahamisha kuwa zaidi ya watu 400 ndio waliojeruhiwa.

Maafisa wa serikali walisema kuwa wanaendelea kufanya uchunguzi wa chanzo na watekelezaji wa mlipuko huo.

İnasemekana kwamba bomu hilo lilikuwa na nguvu isiyokuwa ya kawaida kwenye eneo ambalo hulengwa na kundi la Taliban na wanamgambo waliokuwa na lengo la kudhoofisha serikali ya Afghanistan.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment