Image
Image

ACT.Wazalendo yasema wagombea urais kupitia CCM na UKAWA hawana uwezo wa kupambana na Ufisadi.




Chama cha ACT wazalendo kimewataka watanzania kutodanganyika na sifa wanazo vikwa baadhi ya wagombea wa urais katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi kwani baadhi yao wameshindwa kudhibiti wizi na ubadhirifu wa mali ya umma katika nyadhifa walizokuwa nazo hivyo hawafai kupewa dhamana kubwa ya kuiongoza nchi kwakuwa hakuna jipya watakaloleta zaidi ya kuendeleza uporaji wa mali ya umma
Akihutubia mkutano wa hadhara katika viwanja vya Mwembetogwa mjini Iringa kiongozi wa chama hicho Bwana.Zitto Zuberi Kabwe amesema kumekuwa na maneno mengi ya kuwapamba baadhi ya wagombea wa urais hasa wa vyama vinavyounda umoja wa katiba ya wananchi ukawa na yule wa chama cha mapinduzi CCM lakini hakuna anayefahamu vyema uwezo wa wagombea hao katika kupambana na ufisadi hivyo ni vema wananchi wakawa makini katika kuchagua kiongozi wao.
             BOFYA HAPA KUSIKIA KAULI YA ZITTO KABWE.


Akimzungumzia mgombea wa vyama vinayounda muungano wa ukawa Bwana. Zitto amesema mgombea huyo siyo msafi kama inavyoelezwa na viongozi wa vyama hivyo.

Makada wa chama cha ACT waliohama kutoka chadema na kujiunga na chama hicho hivi karibuni Chiku Abwao na Abuu Changawa walipata tabu kuhutubia mkutano huo baada ya kukumbana na zomea zomea ya wanaodaiwa kuwa ni wafuasi wa Chadema waliokuwa wakipinga hotuba zilizoonekana kuwashambulia viongozi wa chama chao.


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment