Image
Image

Aeleza chanzo cha kuitwa Msaga Sumu.

MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini, Seleman Jabil amefafanua namna alivyopewa jina la Msaga Sumu ambalo sasa linampa umaarufu mkubwa.
Msaga Sumu alisema amepewa jina hilo kutokana na biashara aliyokuwa anaifanya ya kuuza mitumba ambapo anasema kila alipokuwa anafungua mzigo wa nguo alizokuwa anauza alikuwa anapendelea kutoa nguo nzuri na kuziita sumu.
“Hii nguo sumu yaani kila nikifungua mzigo nikikutana na kitu kizuri ni lazima nikiite hivyo hivyo na ndio mwanzo wa kupewa jina la Msaga Sumu ambalo linanipa umaarufu hadi sasa katika tasnia ya muziki ninaoufanya,” alisema.
Katika hatua nyingine, Msaga Sumu alizungumzia muziki anaoufanya ambapo aliweka wazi kuwa kazi zake zinapendwa hadi na mashehe.
“Namshukuru Mungu kazi zangu hazibagui umri zinapendwa na kila mtu chakushangaza zaidi hadi mashehe wanazipenda kwasababu kuna siku nilikuwa nafanya tamasha Mabibo kuna Shehe alinifuta na kuniambia anapenda sana kazi zangu,” alisema
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment