Arsenal yaanza msimu kwa kichapo.
Mabingwa wa FA msimu uliopita na washindi wa kombe la Community Shield wapewa kichapo na Westham
Arsenal walicharazwa kwa mabao 2 bila jibu wakiwa nyumbani emirates katika mechi ya ufungizi ya ligi kuu ya Uingereza.
Mabao ya Westham yalifungwa na Kouyate katika dakika ya 43 na Zarate katika dakika ya 57.
Mlinda lango wa Arsenal aliyesajiliwa kutoka Chelsea Petr Cech alilaumiwa kwa mabao yote mawili.
Katika ujumbe wake wa twitter Cech alisema "Haikuwa ndoto yangu kuanza ligi hivi bali kesho ni siku nyingine ya kujiandaa."
0 comments:
Post a Comment