Image
Image

Man U na Liverpool zaanza vyema, Arsenal na Chelsea zayumba.


Mchakamchaka wa ligi kuu ya soka ya EPL nchini Uingereza ulianza siku ya jumamosi na kuendelea hadi siku ya jumapili kwa mechi kali za kusisimua.
Timu ya Manchester United ilifungua msimu mpya wa EPL kwa mechi kali dhidi ya Tottenham Hotspur iliyochezwa siku ya jumamosi katika uwanja wa Old Trafford, na kuondoka na pointi 3 baada ya ushindi wa 1 – 0.
Siku hiyo hiyo, Chelsea nayo iliponea chupu chupu uwanjani Stamford Bridge baada ya kutoa sare ya 2 – 2 na Swansea City katika mechi waliyolazimika kutamatisha na wachezaji 10. Kipa wa Chelsea Thibaut Courtois, alionyeshwa kadi nyekundu katika dakika ya 52 baada ya kumtendea madhambi msahmbuliaji wa Swansea City, Gomis.
Katika ratiba ya siku ya Jumapili, mabingwa wa taji la FA Cup na Community Shield Arsenal, walijipata matatani baada ya kuaibishwa mbele ya mashabiki na West Ham United. Arsenal walipokea kichapo cha bao 2 – 0 na kuambulia patupu bila pointi yoyote.
Mechi ya mwisho ya siku ya Jumapili ilichezwa kati ya Stoke City na Liverpool ambapo kiungo wa kati Philippe Coutinho aliiokoa Liverpool katika dakika za mwisho na kuiletea pointi 3 baada ya ushindi wa 1 – 0.
Timu ya Manchester City itajitosa uwanjani kupambana na West Bromwich Albion leo usiku katika mechi itakayotamatisha wiki ya kwanza ya EPL.
Matokeo kamili ya mechi za EPL zilizochezwa ni kama ifuatavyo;
Manchester United 1 - 0 Tottenham Hotspur
Bournemouth 0 - 1 Aston Villa
Everton 2 - 2 Watford
Leicester City 4 - 2 Sunderland
Norwich City 1 - 3 Crystal Palace
Chelsea 2 - 2 Swansea City
Arsenal 0 - 2 West Ham United
Newcastle United 2 - 2 Southampton
Stoke City 0 - 1 Liverpool
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment