Image
Image

Dirisha la usajili kufungwa leo.

PILIKAPILIKA za usajili kwa wachezaji wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Ligi Daraja la Kwanza (FDL) na Ligi Daraja la Pili (SDL), zinafikia tamati leo saa 6:00 usiku, imeelezwa. Msemaji wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Baraka Kizuguto alisema kuwa TFF imezikumbusha klabu zote zinazoshiriki msimu mpya wa mwaka 2015/2016, kuhakikisha vinakamilisha usajili wa wachezaji wao kabla ya dirisha hilo la usajili kufungwa.
Kipindi cha dirisha la usajili kwa timu za Ligi Kuu, Daraja la Kwanza na Ligi Daraja la Pili kilifunguliwa Juni 15, 2015 na kitamalizika leo kwa awamu ya kwanza. Timu hasa zile zinazoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara zimekuwa katika heka heka kubwa ya usajili kuhakikisha zinaimarisha zaidi vikosi vyao ili viweze kufanya vizuri katika msimu ujao.
Mbali na kusajili wachezaji wa ndani baadhi ya klabu kama Simba, Yanga na Azam FC wamejiingiza pia katika usajili wa wachezaji kutoka nje ili kuviongezea nguvu vikosi vyao.
TFF imeruhusu wachezaji saba kusajiliwa na klabu za Tanzania na kuweza kuwatumia wote kwa wakati mmoja katika mchezo baada ya msimu uliopita kuruhusu timu kusajili wachezaji watano. Hata hivyo,awali timu ziliomba kuruhusiwa kusajili hadi wachezaji 10 wa kigeni, lakini TFF ikaruhusu wachezaji saba tu.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment