Rais Kikwete ameitumia fursa ya
kuwaaga wakulima na wakazi wa mikoa ya kusini kwa ujumla kwa kuelezea mafanikio
na changamoto mbalimbali katika kipindi chake cha miaka kumi wakati wa kufunga
maonesho ya wakulima maarufu kama nane nane yaliyofanyka kitaifa mkoani Lindi
na kusisitiza kuwa Tanzania ina akiba ya kutosha ya chakula.
Aidh Dr.Kikwete mbali ya kukemea
viongozi aliowaita ni mchwa wanaotafuna fedha za ushirika na kuwafaya wakulima
kukosa masoko ya uhakika ya mazao yao na hivyo kuwafanya kuendelea kuwa
masikini amezungumzia pia suala la mchakato wa kuelekea katika uchaguzi mkuu
kwa kuwataka watanzania kujitokeza kupiga kura na kuhifadhi kadi zao za kupigia
kura na kutokubali kurubuniwa na wajanja wa mitaani.
Rais Kikwete ametumia mtindo wa
kipekee kwa kuwaita baadhi ya mawaziri jukwaani kueleza kile ambacho serikali
yake haijakitekeleza ambapo waziri wa mambo ya nje Mh.Bernard Membe amesema
mahusiano baina ya Tanzania na nchi nyingine ni mazuri na kwamba Tanzania haina
mpango wa kuingia katika vita na nchi yeyote na badala yake hitilafu zozote
za kidiplomasia zitatuliwa kwa njia ya
kidiplomasia.
Katika matukio mengine rais
Dr.Jakaya Mrisho Kikwete amezindu rasmi benki ya maendeleo ya kilimo,kuzindua
mradi wa maji mkoani lindi pamoja na
ujenzi wa nyumba ya mfano za walimu wenye lemgo la kumaliza tatizo la nyumba za
walimu ambapo pia Dr.Magufuli amepata fursa ya kuzungumza na baadhi ya
wanachama wa chama cha mapinduzi katika ofisi za CCM mkoani Lindi kwa kuwaomba
kuwa wamoja licha ya changamoto mbalimbali za kura za maoni.
0 comments:
Post a Comment