Rais MUHAMMADU BUHARI wa Nigeria amesifu jeshi lake la ulinzi kwamba limepata mafanikio makubwa katika kupambana na wapiganaji wa kikundi cha Boko Haramu hasa kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.
Mwishoni mwa ziara yake huko Ghana ambako alikutana na Rais wa nchi hiyo Bwana JOHN
DRAMANI MAHAMA kiongozi huyo wa Nigeria amesema malengo ya mjeshi yake ni kuona kwamba wapiganaji hao hawajiimarishi na kuteka tena miji na vijiji.
Mwezi uliopita Bwana BUHARI aliahidi kuwashinda wapiganaji wa Boko Haram ndani ya miezi mitatu.
Amefahamisha pia kwamba kundi la watu lililotekwa na Boko Haram katika msitu wa Sambisa limegunduliwa lakini bado haijafahamika wazi kama kati ya hao ni wanafunzi wa kike waliotekwa kutoka Chibok mwaka uliopita.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)


0 comments:
Post a Comment