Jaji mkuu wa Tanzania Othmani Chande amekiri bado
kuna mapungufu katika utoaji huduma za mahakama ambapo utafiti unaonyesha kwa
kipindi cha miaka 12 kati ya watu kumi waliotafuta huduma hizo mmoja kati yao
amekumbana na vitendo vya rushwa huku akibainisha katika kipengele cha
uendeshaji wa kesi mahakamani asilimia 48 ya wananchi walohojiwa wamesema
wanaridhika na 45 wakisema kesi zinachukua muda mrefu.
Jaji Chande anatoa takwimu hizo katika mkutano wa
baraza kuu la mahakama ambapo amesema takwimu hizo zimetokana na utafiti
uliofanywa na taasisi ya repoa kwenye mikoa 13 nchini na kuhusisha baadhi ya
mahakama za ngazi zote na kuwahoji wananchi zaidi ya 2000 ambapo umebaini pia
kati ya watu wote waliohojiwa asilimia 82 wameridhishwa na kiwango cha huduma
na asilimia 16 hawakuridhishwa .
Aidha jaji huyo ameelezea hatua mbalimbali
zilizochukuliwa kwa watumishi wasio waadilifu ambapo kwa mwaka 2014/15 pekee
wafanyakazi 22 walishtakiwa kwenye tume ya maadili ambapo 21 kati yao
walifukuzwa kazi kwa kutozingatia maadili.
Kwa upande wao baadhi ya wajumbe wa baraza hilo
wamesema iwapo wananchi hawaridhiki na utendaji wa baadhi ya watumishi wa
mahakama wasisite kutroa taarifa kwani mahakama kama muhimili ina mifumo ya
uendesha ambayo ina fanya kazi na tume ya maadili ya utumishi wa umma.


0 comments:
Post a Comment