Image
Image

Lufthansa yafutilia mbali safari za ndege 1,000 kutokana na mgomo wa marubani.


Shirika la ndege la Lufthansa kutoka Ujerumani limetangaza kufutilia mbali safari za ndege 1,000 kufuatia mgomo wa marubani unaondelea nchini humo.

Shirika hilo limesema kwamba litaweza kutekeleza safari za ndege 500 pekee kati ya 1,520 zilizokuwa zimepangwa siku ya Jumatano kufuatia mgomo wa marubani ulioanza siku ya Jumanne.

Maelezo zaidi yanaarifu kwamba takriban wasafiri 140,000 wameathiriwa na uamuzi huo uliosababishwa na mgomo wa marubani.

Hata hivyo, shirika la Lufthansa limetangaza kwamba shughuli za usafiri kwa washirika wake kama vile Germanwings, Swiss, Austrian Airlines na Brussels Airlines zitaendelea kama kawaida.

Siku ya Jumanne, shirika la Lufthansa lililazimika kufutilia mbali safari za ndege 84 kati ya 170 zilizokuwa zimepangwa kuelekea katika miji ya Frankfurt, Munich na Duesseldorf.


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment