Image
Image

MAGUFULI - Wanaohodhi maeneo ya mashamba bila kuyaendeleza wayaendeleze kama sheria inavyotaka.


Watanzania wanaohodhi maeneo makubwa ya mashamba bila ya kuyaendeleza wametakiwa kuyaendeleza kama sheria inavyotaka la sivyo wajiandae kisaikolojia kwa kuwa watapaswa kuyarejesha ili serikali iweze kuyagawa kwa wananchi wanaohitaji ardhi huku akiahidi kutenga maeneo ya kilimo na mifugo kupunguza migogoro inayoendelea kushamiri baina ya wakulima na wafugaji.

Dr.John Pombe Magufuli ambaye ni mgombea urais kupitia chama cha mapinduzi CCM ameyasema hayo katika wilaya ya ifakara katika mkutano uliohudhuriwa na makumi kwa mamia ya wananchi ambapo amewataka wale wote wanaohodhi mashamba makubwa bila ya kuyaendeleza waanze kuyafanyia kazi la sivyo serikali itayachukuwa yote bila ya kujali wadhifa wa mtu anayeyahodhi ili serikali iyagawe kwa wananchi wenye mahitaji.

Aidha Dr.Magufuli amewahakikishia wananchi wa maeneo ya ifakara,malinyi na mahenge mkoani Morogoro ambapo amefanyaka mikutano ya hadhara kwa kutumia barabara lakini pia kukagu ujenzi wa daraja la mto kilombero na kuwaahidi watanzania kuw serikali yakem itatilia mkazo suala la kuendelea kuboresha miundo mbinu ya barabara.

Mjumbe wa kamati kuu na mwenyekiti wa jumuia ya wazazi CCM Alhaji Abdala Bulembo amewataka watanzania kumchagua Dr. Magufuli kwa kuwa ni mwadilifu na anachukia rushwa na kwamba ana uwezo wa kupambana na mafisadi ambapo pia aliyekuwa diwani na mwenyekiti wa chama cha demokrasia na maendeleo chadema wilaya ya ulanga Bw.Saidi Tira na mratibu wa chadema msingi mkoa wa Morogoro Evance Tagaya wakitangaza rasmi kukihama chama hicho na kujiunga na chama cha mapinduzi CCM.

Dr.Magufuli akiwa njiani kutokea wilaya ya mahenge kwenda ifakara kwa ajili ya kuzungumza na wananchi wa ifakara amekagua ujenzi wa daraja la mto kilombero na kumtaka mkandarasi kuimaliza kazi hiyo kwa wakati ili kuwaondolea wananchi adha wanayoipata kwa sasa. 
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment