Akizindua bodi ya
wadhamini ya mfuko wa fidia kwa wafanyakazi, waziri wa kazi na ajira
Mhe.Gaudencia Kabaka amesema chini ya sheria hiyo waajiri katika sekta binafsi
wanapaswa kuwasilisha michango ya asilimia moja ya jumla ya mishahara ya
wafanyakazi wote ambapo katika sekta ya Umma mwajiri anapaswa kuwasilisha
michango ya asilimia 0.5 katika mfuko huo na kusisitiza sheria hiyo inalenga
kuongeza tija na kumuondolea kazi ya kuhudumia wafanyakazi mwajiri.
Awali akielezea kuhusu
mfuko huo,mwenyekiti wa bodi ya WCF Bwana.Emmanuel Humba amevitaka vyuo vikuu
nchni kuisaidia taasisi hiyo katika kufanya tafiti na kuibua mifumo
itakayosaidia kuendesha mfuko huo kisasa katika utoaji wa huduma katika
mazingira tofauti ya ajari zinazowakuta watumishi wa umma na sekta binafsi hali
itakayosaidia kujenga imani kwa wananchi pamoja na kuongeza uwajibikaji kwa
watendaji.

0 comments:
Post a Comment