Mawakala na wanunuzi wa
Pamba mkoani Shinyanga wametuhumiwa kuua soko la zao hilo nchini kwa kuharibu
ubora wake kwa kuchanganya mchanga,mawe na maji baada ya kununua kutoka kwa
wakulima ili kuongeza uzito hali ambayo imesababisha bei ya pamba kushuka na
kutishia kufungwa kwa wiwanda vya kuchambua pamba na kusababisha ukosefu wa
ajira kwa asilimia kubwa ya wakazi wa mkoa huo.
Akizungumza wakati wa ziara ya ukaguzi
wa viwanda vinavyochambua Pamba mkaguzi mkuu wa Pamba wilayani Kahama
Bw.Emmanuel Kileo amesema pamoja na bodi ya Pamba nchini kutoa elimu juu ya
usafi na ubora wa zao hilo kwa wakulima na wanunuzi lakini bado wahusika
wanafanya makusudi ili mkujipatia maslahi yao binafsi na kusababisha soko la
pamba ya tanzania kuporomoka.
Mmoja wa mawakala anayetuhumiwa kuweka
mawe yenye uzito wa tani tatu katika mzigo wa pamba wenye uzito wa tani kumi na
mbili Bw.Marwa Jackson kutoka katika kampuni ya nida amedai tatizo hilo haliko
upande wake bali ni mipango ya wakulima na wapakiaji kutoka katika maeneo ya
ununuzi kutaka kumharibia kazi yake.
Nao baadhi ya wakulima wa pamba
waliokuja kushuhudia rundo la mawe na mchanga uliokua umechanganywa na pamba
wamesema wanashangaa kusingiziwa kuchafua pamba huku meneja mkuu wa kiwanda cha
kuchambua pamba cha nida Bw.Mohamed Ackbar akiitaka serikali kuunda mfumo mpya
juu ya ununuzi wa pamba kwakua hali hiyo inatishia kufilisi wawekezaji na
kupoteza ajira ya vijana wengi waliokua wameajiriwa katika viwanda vya
kuchambua pamba.


0 comments:
Post a Comment