Wakazi wa Wilaya ya Kakonko Mkoani Kigoma, wamelalamikia kero mbalimbali za maji na barabara inayounganisha mkoa huo na mikoa jirani.
Wamesema kwa zaidi ya miaka hamsini ya uhuru barabara hiyo haijajengwa na hivyo kusababisha kuongezeka kwa ujambazi na utekaji magari pamoja na kutokukua kwa uchumi kutokana na miundombinu duni.
Wakizungumza katika mahojiano na Radio One Stereo wamesema licha ya barabara ya Kigoma-Kasulu kupitia Kakonko hadi Nyakanazi yenye Kilomita 300 kuwa na umuhimu mkubwa kwa uchumi wa Mkoa wa Kigoma na taifa pamoja na ulinzi na usalama kutokana na kuwa mpakani.
Wakazi hao wamewataka viongozi watakaochaguliwa katika uchaguzi mkuu ujao kuipa kipaumbele barabara hiyo ili kurahisisha mawasiliano kati ya Mkoa wa Kigoma na mikoa jirani.
Akizunguzia barabara hiyo katika kampeni za Chama cha Mapinduzi katika Jimbo la Buyungu Kakonko, Waziri wa nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Uwekezaji na Uwezeshaji na mgombea ubunge wa CCM katika jimbo hilo, CHRISTOPHER CHIZA amesema tayari ujenzi wa barabara hiyo umeanza na kwamba mgombea Urais wa CCM Dakta JOHN POMBE MAGUFULI ataikamilisha barabara hiyo baada ya kushika madaraka.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)


0 comments:
Post a Comment