Image
Image

Televisheni ya michezo ya Supersport kuanza kuonyesha mechi za ligi kuu ya soka ya Zambia.


Shirikisho la kandanda nchini Zambia FAZ, limetangaza kutia saini mkataba na televisheni ya michezo ya Supersport kwa ajili ya kuonyesha mechi za ligi kuu ya soka nchini humo.

Mkataba huo wa miaka mitano wa fedha dola milioni 5 utawezesha mechi za ligi kuu ya soka ya Zambia kuonyesha katika televisheni ya Supersport hadi mwaka 2020.

FAZ ilitoa maelezo na kusema kwamba hatua hiyo itasaidia kukuza soka nchini Zambia kutambulisha ligi yao kimataifa.

Mwenyekiti wa FAZ Kalusha Bwalya, alisema kwamba mkataba huo wa miaka mitano pia utahakikishia Zambia fursa mpya za kibiashara za kimataifa zinazohusiana na michezo.


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment