Ofisi ya Waziri Mkuu imewashauri wananchi wakiwemo wadau wa maendeleo, kushiriki kwa ukamilifu kudhibiti na kujiandaa kuzuia maafa yanayo weza kujitokeza kwa taifa pamoja na athari zake ili kuondoa vifo na matatizo yanayoepukika badala ya jukumu hilo kuiachia Serikali pekee.
Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu wa maafa, Ofisi ya Waziri Mkuu, Brigedia-Jenerali MBAZI MSUYA wakati wa uzinduzi wa mpango wa kujiandaa kukabiliana na maafa na zoezi la majaribio kwa halmashauri za Wilaya za Kilosa na Mvomero Mkoani Morogoro.
Ametaja aina ya majanga yanayojitokeza au kulikumba taifa kuwa ni pamoja na mafuriko, milipuko ya mabomu na ugonjwa wa Kipindupindu.
Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, NOELI KAZIMOTO amesema Watanzania wanapaswa kujipanga kwa matatizo ya maafa kwa muda wowote kwani hutokea ghafla bila taarifa.
Mkoa wa Morogoro ni miongoni mwa mikoa inayokabiliwa na majanga ya mafuriko na Kipindupindu mara kwa mara, mambo ambayo yanahitaji jitihada za pamoja katika kudhibiti na kukabiliana na hali hiyo ili kutoleta athari zaidi kwa jamii.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)


0 comments:
Post a Comment