Mamlaka ya Chakula na Dawa - TFDA- imepiga marufuku matumizi ya vipodozi visivyo na kiwango kwa wananfunzi wanaosoma katika shule mbalimbali nchini kwa kuwa vimekuwa vikichangia wanafunzi wengi kupata magonjwa ya ngozi na kujiingiza katika vishawishi.
Akizungumza na wamafunzi wa shule mbalimbali za Sekondari Mkoani Kagera alipokuwa akitoa elimu juu ya madhara ya vipodozi vinavyoingizwa nchini kwa njia za magendo kutoka nchi mbalimbali duniani, Mkaguzi wa Dawa na Vipodozi Kanda ya Ziwa, VENAS BURUSHI amesema vipodozi hivyo vimekuwa na madhara makubwa katika jamii na hasa kwa wasichana wenye umri mdogo.
Katika hatua nyingine Makaguzi Mkuu wa Dawa na vipodozi amebainisha matatizo mbalimbali ambayo mara nyingi yanachangia kuingizwa vipodozi hivyo kwa njiia zisizo halali kuwa ni pamoja na baadhi ya watumishi wa TFDA kurubuniwa na wafanyabiahsara wa vipodozi .
Nao baadhi ya wanfunzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Hekima wameipongeza Mamlaka ya Chakula na Dawa kwa kutambua umuhimu wa wanafunzi kwa kutoa elimu hiyo muhimu na kwamba watakuwa mfano wa kuigwa katika jamii .
Home
Afya
News
TFDA- yapiga marufuku matumizi ya vipodozi visivyo na kiwango kwa wananfunzi nchini Tanzania.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)

0 comments:
Post a Comment