Image
Image

Watu 20 wameuawa na wengine 140 wamejeruhiwa katika mashambulio Boko Haram.

Watu 20 wameuawa na wengine 140 wamejeruhiwa katika mashambulio mawili ya mabomu Kaskazini mwa Cameroon.
Milipuko hiyo ilitokea jimbo la Kerawa ambako jeshi la Cameroon limekuwa linapambana na wapiganaji wa Nigeria wa kikundi cha Boko Haram.
Hivi karibuni kumekuwa na wimbi la mashambulio kaskazini mwa Cameroon yanayolaumiwa kufanywa na wapiganaji wa Jihadi wa kikundi hicho cha Boko Haram.
Mlipuko wa bomu la kwanza ulitokea kwenye soko la Kerawa na wa pili baadaye kiasi cha mita 200 kutoka kambi ya jeshi la nchi kavu na baadhi ya taarifa zinasema watu wapatao 30 wameuawa.


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment