Image
Image

Watu 20 wameuawa wengi wamejeruhiwa katika mji mkuu wa Yemen, Sanaa.

Watu 20 wameuawa na wengine wengi wamejeruhiwa,kufuatisha shambulio la bomu la kujitoa muhanga kwenye msikiti mmoja wa madhehebu ya Shia katika mji mkuu wa Yemen, Sanaa.
Mashuhuda wanasema mtu wa kujitoa muhanga alijilipua wakati waumini wakitokea msikitini na wapiganaji wa jihadi wa kikundi cha Islamic State wamedai kuhusika na shambulio hilo.

Mapema wafanyakazi wawili wa misaada waliuawa kwa kupigwa risasi,  na Chama cha Msalaba Mwekundu kimesema wafanyakazi wake hao wawili wameua wakiwa katika msafara mjini Sanaa.
Inasadikiwa mtu mwenye bunduki alilifyatulia gari lao wakati wanasafiri kupitia jimbo la Kaskazini la Amran,  wakati wakitokea Saada,  ngome ya waasi wa Houthi.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment