Image
Image

FUNUNU:Baraza la Mawaziri kutangazwa muda wowote kuanzia hivi sasa.



Muda si mrefu Rais wa Tanzania awamu ya Tano Dkt.John Pombe Magufuli amewaita wanahabari Ofisini kwake kwa lengo la kuzungumza nao lakini haijafahamika mara moja nini  anataka kuzungumza nao.

Licha yakuwa haijabainika ninini anachotaka kusema lakini kwa fununu na hamu iliyokuwa kubwa kwa watanzania wanabashiri kuwa huenda akaliweka wazi baraza la mawaziri ambalo amekuwa akisema anataka liwe dogo na lenye watendaji kazi wazuri ndani ya serikali yake ya awamu ya Tano yenye kaulimbiu ya Hapa kazi tu.

Tangu kuchaguliwa kuwa Rais wa Tanzania ameweza kufanya mambo mazito ndani ya nchi haswa kwa kugusa sehemu nyeti ndani ya serikali hali ambayo imekuwa ikimfanya apate sifa ndani na nje ya nchi huku wengine katika nchi zao wakitamani akawe rais katika nchi zao kwa kile wanachotaja kuwa sasa Tanzania imepata mkombozi.

Licha ya kuwa hajatangaza baraza la mawaziri Rais Magufuli lakini nchi imekwenda vizuri kwa kuwa na Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa,Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan,Mwanasheria mkuu wa Serikali George Masaju,Spika wa Bunge Mh.Job Ndugai na Naibu Spika Tulia Ackson Mwansasu.

Kasi ya Rais Magufuli na Waziri wake imekuwa kubwa kwa kutumbua Majipu katika Mamlaka za Kodi TRA na Mamlaka ya Bandari TPA, na kulazimika kufuta Sherehe za Uhuru,Siku ya Maadhimisho ya Ukimwi,Kufuta Safari za Nje nk.Kusudi kubana matumizi ya sio kuwa na Tija.

Itakavyokuwa baada ya Mazungumzo tutakufahamisha kilicho jiri.


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment