Image
Image

Micho:Ukweli nikwamba Kili Stars ndiyo timu bora Chalenji.

Kocha wa timu ya soka ya Taifa ya Uganda (The Cranes), Milutin Sredojevic ‘Micho’ (pichani)ameitaja timu ya Tanzania Bara (Kilimanjaro Stars) kuwa ni ndiyo timu ambayo hakutaka kukutana nayo kwenye hatua ya robo-fainali ya mashindano ya Kombe la Chalenji yanayoendelea nchini Ethiopia.

Mserbia alisema jana kuwa kikosi cha Stars amekishuhudia kwenye michuano hiyo kikiwa na ubora kwenye kila idara na anakipa nafasi kubwa ya kutinga fainali.

“Katika hatua ya robo-fainali niliomba Mungu tusikutane na Kilimanjaro Stars, ndiyo timu ngumu ninayoiona mpaka sasa. Ina mabeki makini, viungo wabunifu na washambuliaji wenye kasi na uwezo mzuri wa kushambulia,” alisema Micho.

Kocha huyo wa zamani wa Yanga, alisema kuwa safu ya kiungo ya Stars ndiyo inayofanya kazi kubwa zaidi kiasi cha kuifanya timu hiyo kukusanya pointi saba katika mechi tatu za hatua ya makundi.

Uganda itacheza mechi yake ya robo-fainali ya michuano hiyo dhidi ya timu mwalikwa, Malawi kwenye Uwanja wa Addis Ababa kabla ya Stars kuwakabili wenyeji, timu ya taifa ya Ethiopia.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment