Image
Image

Watumishi wa manispaa ya Kagera waamriwa kufunga ofisi na kufanya usafi.

Mkuu wa Mkoa wa Kagera,JOHN  MO NGELLA amewataka watumishi wote manispaa hiyo kufunga ofisi na kuingia mtaani kufanya usafi wa mazingira kutokana uzembe uliofanywa na Maofisa Afya wa manispaa hiyo kwa kushindwa kusimamia kwa ukamilifu  suala usafia wa mazingira.
Ametoa agizo hilo  baada ya kupokea vifaa vya usafi vilivyotolewa na Shirika la  Hisani la  World Vision kwa lengo la kukabilana na uogonjwa  wa Kipindupindu ambao umekuwa tishio kwa wananchi .
Mkuu huyo wa Mkoa wa Kagera ameamuru watumishi wote wa Manispaa  ya Bukoba  kwa  kushirikiana na  wananchi kuwajibika kufanya usafi wa mazingira katika Mtaa wa Bunena,Kashabo na Buyekela,mitaa ambayo  imetajwa kuongoza  kwa kuwa na idadi kubwa ya wagonjwa wa Kipindupindu kutoka na  na ongezeko la uchafu katika maeneo hayo .
Kwa upande wake Mganga Mkuu wa wilaya,Dakta   HAMZA MUGULA amesema jitihada za kupambana na ugnjwa huo zinaendelea kwa kasi kubwa na kuongeza kuwa taangu tarehe 13 Oktoba mwaka huu hadi sasa wamepokea wangonjwa wa   Kipindupindu zaidi ya miamoja na kati hao wawili walipoteza maisha.


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment