Image
Image

Zifahamu hapa faida ya kutumia chenza kila mara kiafya.


Chenza ni moja ya tunda lenye ladha nzuri sana na lenye kupendwa na watu wengi wakiwemo watoto na watu wazima pia.
Tunda hili wengi wetu tumekuwa tukilitumia sana huenda kutokana na kupenda ladha yake tu, lakini hili ni moja ya tunda ambalo pia lina faida nyingi katika miili yetu.
Miongoni mwa faida za chenza ni pamoja na kusaidia kuongeza vitamin C mwilini kama ilivyo katika chungwa, pia husaidia kuongeza nguvu kwenye misuli na kuimarisha mifupa.
Tunda hili pia husaidia kuzuia uvujaji wa damu katika fizi, na huondoa maumivu ya viungo sambamba na kuwasaidia wale wenye udhaifu wa kuona.
Mbali na hayo, pia chenza huwasidia wale wenye tatizo la mawe ya figo na kibofu, viuvimbe chini ya tumbo na inatibu unene wa mirija ya damu.
Matumizi yake katika tiba ni wewe kuzingatia kula kila unapoweza kulipata tunda lake.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment