Image
Image

Chama cha Madaktari wa kinywa na meno wafanya zoezi la uchunguzi kinywa na Meno.


Chama cha madaktari wa kinywa na meno nchini kwa kushirikiana na wadau wengine kimefanya zoezi la uchunguzi wa afya ya kinywa na meno pamoja na kutoa elimu kwa watoto wapatao 258 katika shule ya msingi maalum buguruni jijini dar es salaam.
Akizungumza na itv mratibu wa zoezi hilo Bi.lizabeth Limo amesema mbali na kufanya uchunguzi katika shule hiyo pia wanalenga kumsaidia mtoto kutambua ni jinsigani anaweza kutunza kinywa pamoja na meno dhidi ya magonjwa ambayo yanaweza kuepukika kwa kufuata njia sahihi katika usafishaji.
Kwa upande wake makamu mkuu wa shule Bw,George Njau amesema anashukuru kwa zoezi hilo kufanyika shuleni hapo kwani kutasaidia katika kuboresha afya ya kinywa na meno kwa wanafunzi hoa na kutoa wito kwa wadau mbalimbali katika kuwasaidia watoto wenye uhitaji maalum kwani nao wana haki ya kupata huduma zote muhimu
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment