Image
Image

Machafuko baada ya uchaguzi Uganda yaua watu 22.

Polisi ya Uganda imetangaza kuwa mapigano yaliyojiri magharibi mwa nchi hiyo kati ya wafuasi wa wagombea uchaguzi wanaohasimiana ambao walishiriki katika uchaguzi mkuu wa nchi hiyo yameuwa watu 22 na kuwajeruhi wengine 10.
Chama cha upinzani cha Mabadiliko ya Demokrasia (FDC) kimeituhumu serikali ya Uganda kuwa imechochea machafuko hivi karibuni katika eneo ambalo mgombea wa upande wa upinzani Kizza Besigye ana uungaji mkono mkubwa dhidi ya kiongozi mkongwe Yoweri Museveni ambaye alishinda uchaguzi wa rais uliofanyika nchini humo tarehe 18 Februari huku ukigubikwa na udanganyifu.
Polisi ya Uganda ilisema katika taarifa iliyotoa jana kuwa ghasia ziliibuka kati ya wafuasi wa wagombea hasimu baada ya kufanyika uchaguzi wa serikali za mitaa katika eneo hilo tarehe 24 Februari. Polisi imesema kuwa raia 16 waliaga dunia kwenye machafuko kati ya wafuasi wa wagombea hao wanaohasimiana, na wengine 6 waliaga dunia baada ya polisi kuingilia kati ili kuzima ghasia hizo. Mbali na kuuawa watu hao, watu wengine 10 walijeruhiwa wakiwemo wanajeshi wanne, huku nyumba 149 zikichomwa moto.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment