Image
Image

Serikali yatoa Milioni 200 kukamilisha ujenzi wa daraja la Mto Kilombero.




Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi,na Mawasiliano,Profesa MAKAME MBARAWA amesema Serikali imetoa Shilingi BILIONI  11 na Milioni  2 00  kukamilisha haraka ujenzi wa Daraja la Mto Kilombero .
Daraja hilo lenye urefu wa Mita 384 linatarajiwa kukamilika novemba 11 mwaka huu na kuepusha wananchi kupata adha ya kivuko ya mara kwa mara inayogharimu maisha ya watu na upotevu wa mali.
Akizungumza na wananchi wa Kilombero na Ulanga wakati akitembelea kivuko kilicho pata ajali mapema mwaka huu na kugharimu maisha ya watu na upotevu wa mali,Profesa MBARAWA amesema serikali itahakikisha daraja lina kw isha mapema na kuwaondolea adha wananchi wa wilaya hizo na  wavuke kwa usalama zaidi .
Kwa upande wao wananchi wa Kilombero na Ulanga wameiomba serikali kuharakisha ujenzi wa daraja hilo kwani kivuko kilichopo bado si o  salama na kumekuwa kukitokea matukio mengi ya kuzama kwa kivuko n a kupoteza ndugu zao.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment