Image
Image

Mahakama nchini CAR yaidhinisha ushindi wa Faustin.

Mahkama ya katiba nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati imeidhinisha ushindi wa rais mpya wa nchi hiyo Faustin-Archange Touadéra.
Mahakama hiyo ilitoa ripoti hiyo jana na kumtangaza mwanasiasa huyo kuwa ni rais mpya wa nchi hiyo aliyeibuka mshindi katika duru ya pili ya uchaguzi wa rais hapo tarehe 14 Februari. Zacharie Ndouba, mkuu wa mahkama ya katiba ameunga mkono matokeo ya uchaguzi yaliyotangazwa tarehe 20 Februari na Tume ya Uchaguzi (ANE) na kusisitiza kuwa, Faustin-Archange Touadéra ndiye rais halali aliyechaguliwa na wananchi wa Jamhuri ya Afrika ya Kati kwa kupata asilimia 62.69 ya kura dhidi ya mshindani wake Anicet-Georges Dologuélé. Aidha imetupilia mbali maombi yoyote ya kutaka kubatilishwa matokeo ya duru ya pili ya uchaguzi wa rais wa nchi hiyo. Hatua hiyo imekuja baada ya Anicet-Georges Dologuélé kutuhumu kuwepo uchakachuaji mkubwa katika uchaguzi huo na hivyo kuitaka mahakama hiyo ya katiba kutupilia mbali matokeo hayo.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment