Image
Image

Rais Zuma wa Afrika Kusini amenusurika kwa mara ya pili kuondolewa madarakani kwa kura.

Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini amenusurika kwa mara ya pili katika kipindi cha mwaka mmoja kuondolewa madarakani kwa kura ya kutokuwa na imani naye, baada ya hoja iliyowasilishwa bungeni kutoungwa mkono na wabunge walio wengi.
Hoja hiyo ya tuhuma dhidi ya Zuma ya utendaji mbovu wa kiuchumi iliwasilishwa bungeni na chama kikuu cha upinzani Muungano wa Kidemokrasia (DA) na kupigiwa kura hapo jana. Hata hivyo Rais wa Afrika Kusini alishinda hoja hiyo kutokana na uungaji mkono wa chama chake tawala cha ANC ambacho kinahodhi karibu thuluthi mbili ya viti vyote vya bunge la nchi hiyo.
Wabunge 225 walipiga kura ya kupinga hoja hiyo ya kutokuwa na imani na utendaji wa kiuchumi wa Zuma iliyoungwa mkono na wabunge 99 mbali na 22 walioamua kutopiga kura. Rais wa Afrika Kusini mwenyewe hakuhudhuria kikao hicho cha bunge.
Akizungumza katika kwa niaba ya chama kikuu cha upinzani, Waziri kivuli wa Fedha David Maynier aliliambia bunge lililokuwa likirusha moja kwa moja kikao hicho kupitia televisheni ya taifa kuwa Rais Zuma amekuwa mvurugaji wa uchumi ambaye hatosita kufanya lolote ili kuweza kuendelea kubaki madarakani ikiwemo kubomoa uchumi na kuibomoa Afrika Kusini yenyewe.
Kiongozi wa chama hicho cha Muungano wa Kidemokrasia Mmusi Maimane alitoa wito wa kuondolewa madarakani Zuma akiashiria Waafrika Kusini milioni nane na laki mbili ambao amesema hawana ajira.
Licha ya tuhuma hizo, Waziri wa serikali Bi Lindiwe Zulu aliliambia bunge katika mjadala uliochukua takribani muda wa masaa matatu kwamba Jamii ya Kimataifa ina imani na Rais Zuma.
Daryl Glaser, mchambuzi wa siasa katika Chuo Kikuu cha Wits amesema kwa hatua yao hiyo, wapinzani wanatumai kudhoofisha nafasi ya Zuma mbele ya umma na vilevile kuzidisha mpasuko ndani ya chama tawala
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment